-
Angola: Kilichokwamisha mazungumzo ya Jumanne baina ya serikali ya DRC na M23 ni nguvu za kigeni
Mar 20, 2025 03:11Wizara ya Mambo ya Nje ya Angola imesema kuwa mazungumzo ya amani kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na kundi la waasi la March 23 ambayo yalipangwa kufanyika juzi Jumanne, yalisitishwa kutokana na ushawishi wa nguvu za nje.
-
AU yalaani shambulio dhidi ya msafara wa Rais wa Somalia
Mar 19, 2025 23:41Somalia na Umoja wa Afrika (AU) zimelaani shambulizi la kigaidi lililolenga msafara wa Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud huko Mogadishu, mji mkuu wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
M23: Hatutaki kingine ghairi ya amani nchini Kongo DR
Mar 19, 2025 23:39Muungano wa Mto Congo (AFC) na tawi lake la waasi wa M23 zinasisitiza kuwa, lengo lao kuu ni amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, lakini zinadai kuwa, kufikiwa kwake kunakwamishwa na mashambulizi ya serikali.
-
Rais wa Nigeria atangaza hali ya dharura katika jimbo lenye utajiri wa mafuta, amtimua gavana
Mar 19, 2025 08:38Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, ametangaza hali ya dharura katika eneo lenye utajiri wa mafuta la Rivers kufuatia mgogoro wa kisiasa uliodumu kwa muda mrefu na utawala mbaya.
-
Rais wa Somalia anusurika jaribio la mauaji la magaidi wa al-Shabaab
Mar 19, 2025 08:23Serikali ya Somalia imetangaza kuwa mlipuko uliofanyika Jumanne mjini Mogadishu ulikuwa jaribio la kumuua rais wa nchi hiyo ambalo limetekelezwa na kundi la kigaidi la al-Shabaab.
-
Amiri wa Qatar awakutanisha viongozi wa DRC na Rwanda huku mvutano ukishadidi
Mar 19, 2025 08:20Amiri wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani amewaleta pamoja viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Rwanda kwa lengo la kutuliza hali mashariki mwa DRC.
-
Afisa wa UN: Sudan Kusini iko kwenye ukingo wa vita vya wenyewe kwa wenyewe
Mar 19, 2025 04:13Mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, Nicholas Haysom, ameonya kwamba nchi hiyo inaweza kurejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya mapigano yaliyotokea kaskazini mashariki mwa nchi kulazimisha maelfu ya watu kuyahama makazi yao, huku balozi kadhaa za Magharibi kujitolea kufanya upatanishi ili kuzuia hali kuwa mbaya zaidi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan: Mpango wa kuanzisha serikali nyingine mezaliwa ukiwa maiti
Mar 19, 2025 04:13Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Sudan amesema mpango wa makundi ya upinzani yakiongozwa na Rapid Support Forces (RSF) wa kuunda serikali nyingine nchini Sudan umezaliwa ukiwa maiti.
-
Niger yajitoa rasmi katika Jumuiya ya Nchi Zinazozungumza Kifaransa, Francophone
Mar 19, 2025 00:44Niger imejiondoa rasmi katika Jumuiya ya Kimataifa ya nchi zinazozungumza Kifaransa (OIF) au Francophone sambamba na juhudi zinazoendelea kufanywa na taifa hilo la Afrika Magharibi za kuvunja uhusiano na kujitenga na mkoloni wake wa zamani, Ufaransa.
-
Shambulio la RSF laua raia wanne na kujeruhi wanane katika mji wa Omdurman, Sudan
Mar 19, 2025 00:43Wizara ya Afya ya Sudan imetangaza kuwa, raia wanane wameuawa na wengine wanne wamejeruhiwa katika shambulizi la mizinga lililofanywa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) huko Omdurman, mji mkuu pacha wa nchi hiyo Khartoum.