Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad katika ziara rasmi ya kikazi yenye lengo la kuimarisha usalama na uhusiano wa kibiashara kati ya nchi mbili.
Harakati ya Mapamabano ya Kiislamu (Muqawama) ya Hizbullah ya Lebanon imesema wapiganaji wake wameiangusha ndege ya kisasa isiyo na rubani ya kivita na kijasusi ya utawala haramu wa Israel kusini mwa Lebanon baada ya kukiuka anga ya nchi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Jamhuri ya Kiislamu iliikuwa imeshaitaarifu serikali ya Marekani kabla ya kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel mfanyamauaji ya kimbari.
Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vinazikanusha picha na mikanda ya video inayosambazwa na vyombo kadhaa vya habari, ikionyesha maeneo tofauti ndani ya utawala huo yaliyolengwa na makombora ya Iran ikiwa ni kufuata na kutekeleza sera ya habari ya baraza la mawaziri la vita la utawala huo haramu.
Wananchi konte nchini Iran wamejitokeza mitaani kuunga mkono hatua ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ya kuuadhibu utawala wa Kizayuni wa Israel kufuatia kitendo chake cha kichokozi cha kutekeleza mashambilizi ya kigaidi dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran jijini Damascus Aprili Mosi.
Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya ughaibuni ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Khaled Mash'al, amepongeza istiqama ya kishujaa ya Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa vita vya miezi sita wanavyopigana Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel "karibuni hivi vitamvunja adui Mzayuni".
Klipu hii ina maelezo ya makombora tisa ya kisasa kabisa ya Iran yenye usahihi wa hali ya juu ambayo yameuingiza woga utawala wa Kizayuni wa Israel.
Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amesema kuwa, nchi yake itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki utakaofanyika mwezi ujao wa Mei.
Masheikh wawili maarufu wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamezungumzia umuhimu wa Siku ya Kimataifa ya Quds na uungaji mkono wa Waislamu wa nchi hiyo kwa kadhia nzima ya Palestina hususan Ghaza.
Wananchi huko Italia, Norway, Marekani, Japan na Morocco kwa mara nyingine tena wameandamana kulaani mauaji ya kimbari ya raia wa Palestina yanayofanywa na wanajeshi ghasibu wa utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza.