Rais wa Iran: Walimwengu watajionea kuangamia kwa utawala wa Kizayuni
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu maalumu za kuwashukuru wananchi walio macho na wenye kujali thamani ya mambo wa Iran kwa ushiriki wao mkubwa katika matembezi ya Siku ya Quds Duniani na kusema: Walimwengu watajionea kuangamia kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
Kwa mujibu wa Shirika Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB, katika salamu zake, Rais Ebrahim Raisi, amepongeza kushiriki kwa ukakamavu wananchi walio macho na wenye kujali thamani ya mambo wa Iran na akasema, mahudhurio hayo yanatuma ujumbe wa wazi kwa Uistikbari duniani kwamba, mwisho wa dhulma na uporaji, uchokozi na mauaji huwa ni kushindwa tu.
Jana, Ijumaa, Aprili 5, 2024 sawa na Ramadhani 25, 1445, ilikuwa Siku ya Kimataifa ya Quds.
Matembezi ya Siku ya Quds Duniani jana Ijumaa yalifanyika katika miji na vijiji zaidi ya elfu mbili nchini Iran kwa kuhudhuriwa na wananchi wakakamavu wa Iran.../