Wakazi wa mji mkuu wa Iran watoa heshima za mwisho kwa Ebrahim Raisi na wenzake
May 22, 2024 07:23 UTC
Wananchi na wakazi wa mji wa Tehran leo wametoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa Ebrahim Rais pamoja na wenzake walioaga dunia katika ajali ya helikopta siku ya Jumapili.
Umati mkubwa wa watu umejitokeza asubuhi ya leo hapa mjini Tehran kwa ajili ya kuaga miili ya mashahidi hao akkiwemo Rais Ebrahim Rais na waziri wake wa Mashauri ya Kiigeni Hussein Amir-Abdollahian. Nimezungumza na mtangazaji mwenzetu Amir Ibrahim Rutajengwa ambaye ameshiriki katika shughuli hiyo na alikuwa na haya ya kusema…