Rais Pezeshkian: Tutajenga upya kila kilichoharibiwa, tena bora kuliko hapo awali
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i137392-rais_pezeshkian_tutajenga_upya_kila_kilichoharibiwa_tena_bora_kuliko_hapo_awali
Rais wa Iran amesisitiza kuwa, “Kwa msaada wenu, watu watukufu wa Iran, tutavuka kipindi hiki na tutajenga upya kila kilichoharibiwa, tena bora zaidi kuliko hapo awali.”
(last modified 2026-03-27T07:58:19+00:00 )
Mar 16, 2026 04:12 UTC
  • Rais Pezeshkian: Tutajenga upya kila kilichoharibiwa, tena bora kuliko hapo awali

Rais wa Iran amesisitiza kuwa, “Kwa msaada wenu, watu watukufu wa Iran, tutavuka kipindi hiki na tutajenga upya kila kilichoharibiwa, tena bora zaidi kuliko hapo awali.”

Kwa mujibu wa Pars Today, Rais Masoud Pezeshkian ameandika katika ujumbe aliouchapisha kwenye jukwaa la kijamii X Jumamosi kwamba: “Siku kumi na tano zimepita tangu vita vya kikatili vilivyolazimishwa vianze. Licha ya changamoto katika usafiri, mawasiliano na maeneo mengine, kutokana na juhudi za wenzetu serikalini, hakuna usumbufu mkubwa uliotokea katika utoaji wa huduma kwa wananchi wa Iran.”

Amesisitiza: “Kwa ushirikiano wenu, watu watukufu wa Iran, tutashinda hali hii na tutajenga upya kila walichoharibu, kwa namna iliyo bora zaidi kuliko hapo awali.”

Rais hapo awali pia, katika sehemu ya ujumbe wake wa kuwashukuru wananchi kwa ushiriki wao katika maandamano ya Siku ya Quds, alikumbusha kuwa: “Leo, pamoja na maandalizi yanayohitajika kwa ajili ya ulinzi wa kina wa vikosi vya ulinzi vya nchi, jambo kuu linaloipa serikali wasiwasi ni kupanga na kusimamia vyema masuala ya maisha ya wananchi. Ushirikiano, mshikamano na ushiriki wa mihimili yote ya dola ni muhimu ili kujibu ipasavyo changamoto hizi.”

Pia alieleza kuwa uungwaji mkono wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ni rasilimali kubwa kwa serikali, na mzigo mzito wa kuendesha nchi unahitaji msaada wake. Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwa kutegemea mtaji wake mkuu ambao ni uungwaji mkono wa wananchi pamoja na uongozi wa Kiongozi Muadhmu, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu itaweza kuondoa vikwazo vilivyopo njiani na kufanikiwa katika kutekeleza majukumu yake na kutoa huduma kwa taifa kubwa la Iran katika kipindi hiki kigumu.