IAEA yasisitizia, Iran imeheshimu makubaliano ya JCPOA
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i19189-iaea_yasisitizia_iran_imeheshimu_makubaliano_ya_jcpoa
Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) umesisitiza tena katika ripoti yake mpya kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetekeleza na kuheshimu makubaliano ya nyuklia maarufu kama JCPOA kwa kifupi.
(last modified 2026-02-21T22:51:18+00:00 )
Nov 10, 2016 04:27 UTC
  • IAEA yasisitizia, Iran imeheshimu makubaliano ya JCPOA

Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) umesisitiza tena katika ripoti yake mpya kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetekeleza na kuheshimu makubaliano ya nyuklia maarufu kama JCPOA kwa kifupi.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, Yukia Amano amesisitiza katika ripoti yake mpya kuhusu makubaliano ya miradi ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1 kwamba, Tehran imetekeleza makubaliano hayo.

Baada ya kutolewa ripoti hiyo ya msimu, mwakilishi wa Iran katika Wakala wa IAEA, Reza Najafi amesema kuwa, ripoti mpya ya Yukia Amano imethibitisha tena kwamba, Iran imetekeleza kikamilifu makubaliano ya JCPOA.

Image Caption

Najafi ameongeza kuwa, ripoti hiyo imeonesha tena kwamba, miradi ya kuzalisha nishati ya nyuklia nchini Iran inafanyika kwa mujibu wa sheria za kimataifa na makubaliano ya JCPOA katika sekta sote za kurutubisha madini ya urani, uhakiki na utafiti, ujenzi mpya wa kinu cha nyuklia cha Arak na uzalishaji wa maji mazito.