-
Russia yawafukuza nchini wanadiplomasia sita wa Uingereza kwa ujasusi
Sep 14, 2024 01:05Russia imewafukuza nchini humo wanadiplomasia sita wa Uingereza kwa kufanya ujasusi. Russia imechukua hatua hiyo ili kulipiza kisasi kwa vikwazo vipya vya Marekani na Uingereza dhidi yake.
-
Rais wa Iran: Israel haitathubutu kutenda jinai kama Waislamu wataungana
Sep 14, 2024 00:54Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa iwapo Waislamu watashirikiana na kuwa kitu kimoja utawala wa Israel hautathubutu kufanya mauaji ya umati dhidi yao. Rais Masoud Pezeshkian ameeleza haya alipokutana na kuzungumza jana huko Basra Iraq na wasomi wa kitamaduni, kidini, kielimu na wengineo.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Umoja ni kipaumbele cha ulimwengu wa Kiislamu
Sep 13, 2024 08:15Khatibu wa muda wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema: "Umoja ni moja ya vipaumbele vya Ulimwengu wa Kiislamu na ndiyo maana silaha muhimu ya adui katika kueneza ukoloni ni kuibua mifarakano."
-
Iran yapendekeza muungano wa kupambana na vikwazo ili kuhakikisha usalama wa biashara katika BRICS
Sep 13, 2024 04:04Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Taifa la Iran (SNSC) Ali Akbar Ahmadian ametoa wito wa kuanzishwa muungano wa kukabiliana na vikwazo ili kukuza biashara na usalama wa kifedha kati ya kundi la BRICS la nchi zinazoinukia kiuchumi.
-
Iran yakanusha madai ya kujaribu kuwamaliza wapinzani nje ya nchi
Sep 13, 2024 04:02Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York amepinga vikali madai ya kuwepo majaribio ya kuwamaliza wapinzani wa Jamhuri ya Kiislamu nje ya nchi akiyataja kuwa ni "uzushi" uliobuniwa na maadui.
-
Iran yalaani shambulio la Israel dhidi ya skuli ya UN Gaza
Sep 12, 2024 23:35Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani shambulizi la anga la Israel dhidi ya shule nyingine iliyogeuzwa makazi na wakimbizi katika Ukanda wa Gaza, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 18, wakiwemo wafanyakazi sita wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Radiamali ya Iran kwa vikwazo vya nchi za Ulaya dhidi ya Shirika la Ndege la Iran Air
Sep 12, 2024 23:00Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ameichukulia kauli ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani kuhusiana na kufutwa makubaliano ya pande mbili ya kutoa huduma za anga kwa Iran kuwa ni ugaidi wa kiuchumi wa nchi za Magharibi dhidi ya taifa la Iran.
-
Kuongezeka mauzo ya bidhaa za Iran nchini Iraq
Sep 12, 2024 08:04Shirika la Maendeleo ya Biashara la Iran limetangaza kuwepo ongezeko kubwa la mauzo ya Iran nchini Iraq katika miezi ya karibuni.
-
Iran yaazimia kuimarisha uhusiano na Burkina Faso
Sep 12, 2024 07:37Balozi wa Iran nchini Burkina Faso, Mojtaba Faqihi amekutana na Abubakar Nakanabo, Waziri wa Uchumi na Fedha wa taifa hilo la Afrika Magharibi na kujadili umuhimu wa kupanua ushirikiano wa pande mbili katika nyuga za kiuchumi, kiufundi na kibiashara.
-
Iran: Marekani na Uingereza ndio wachochezi wakuu wa vita duniani
Sep 12, 2024 07:36Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema Marekani na Uingereza ndio wachochezi wakuu wa moja kwa moja na wasio wa moja kwa moja wa kila vita vinavyotokea katika pembe yoyote duniani.