-
Samia amwapisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Tanzania
Nov 14, 2025 07:42Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amemwapisha Dk. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuthibitishwa na Bunge jana Alkhamisi Novemba 13, 2025.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Congo DR: Rwanda lazima ionyeshe hamu ya kweli ya kutaka amani
Nov 14, 2025 06:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Thérèse Kayikwamba Wagner, ameikosoa vikali Rwanda, akiitaka ithibitishe dhamira yake ya kweli ya kutaka amani, kutokana na uwepo wa vikosi vyake ndani ya ardhi ya Congo na mvutano unaoongezeka mashariki mwa nchi hiyo.
-
Jarida la Wall Street: Makampuni ya Marekani yalipata mabilioni ya dola kutokana na vita dhidi ya Gaza
Nov 14, 2025 06:18Jarida la Wall Street limefichua kwamba vita vya miaka miwili vya Ukanda wa Gaza havikuwa tu janga kubwa la binadamu, bali pia muamala mkubwa wa biashara kwa makampuni ya Marekani yaliyopata mabilioni ya dola kutokana na mauzo ya silaha kwa Israel, kwa msaada mpana wa kisiasa na kiuchumi kutoka Washington.
-
CDC: Afrika inakabiliwa na mlipuko mbaya zaidi wa kipindupindu katika miaka 25
Nov 14, 2025 06:09Shirika la Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika (CDC) limetahadharisha kuwa bara la Afrika linakabiliwa na mlipuko mbaya zaidi wa kipindupindu katika kipindi cha robo karne, likifungamanisha ongezeko hilo na miundombinu dhaifu ya maji na migogoro inayoendelea katika sehemu mbalimbali za bara hilo.
-
Baraza la Haki za Binadamu la UN linapigia kura rasimu ya azimio kuhusu Sudan
Nov 14, 2025 05:41Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa leo Ijumaa, litapiga kura katika kikao maalumu kinachojadili mgogoro wa Sudan, kuhusu rasimu ya azimio linalolaani ukiukwaji wa haki za binadamu ambao linasema umefanywa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) ndani na karibu na mji wa El Fasher katika shambulio la hivi karibuni la wapiganaji wa kundi hilo dhidi ya mjini huo.
-
Kwa nini kutoshiriki Marekani katika kikao cha G20 nchini Afrika Kusini ni hasara kubwa kwa Washington?
Nov 14, 2025 04:39Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amesisitiza kuwa kutohudhuria Wamarekani katika kikao cha G20 ni hasara kubwa kwao.
-
Iran na Uturuki zatilia mkazo kupunguzwa mivutano na kurejeshwa amani na uthabiti katika eneo
Nov 14, 2025 04:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyidd Abbas Araqchi, amefanya mazunguzmo kwa njia ya simu na mwenzake wa Uturuki Hakan Fidan, ambapo wawili hao wamejadili uhusiano wa pande mbili na matukio ya kikanda na kimataifa.
-
Maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni zagunduliwa Ghaza
Nov 14, 2025 04:13Timu za uokoaji za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimegundua na kufukua maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
UN yamchagua Profesa Phoebe Okowa wa Kenya kuwa Jaji wa Mahakama ya ICJ
Nov 14, 2025 04:12Katika kura ya kihistoria iliyopigwa Umoja wa Mataifa siku ya Alkhamisi, profesa wa sheria wa Kenya Phoebe Okowa alichaguliwa kuwa jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), akiibuka mshindi kwenye ulingo wa ushindani wa wagombea wa Kiafrika baada ya mfululizo wa raundi za kupiga kura zilizokuwa na mvutano katika Baraza Kuu na Baraza la Usalama.
-
Vitisho vya mzayuni vyaifanya serikali ya Al-Jolani ifute maadhimisho ya Kimbunga cha Al-Aqsa
Nov 14, 2025 04:08Duru za habari zimeripoti kuwa kongamano la Operesheni ya Muqawama wa Palestina dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel ya Kimbunga cha Al-Aqsa, lililokuwa limepangwa kufanyika katika mji wa Aleppo nchini Syria limefutwa baada ya mwandishi mmoja wa habari wa Kizayuni kutoa vitisho kwa kiongozi wa mpito wa nchi hiyo, Al-Jolani na serikali yake.