Oct 05, 2024 12:38 UTC
  • Wazayuni wafanya mashambulizi makubwa katika  hospitali moja huko  mjini Beirut

Wavamizi wa Kizayuni wamelenga hospitali ya Bint Jbeil iliyoko kusini mwa Lebanon.

Kulingana na ripoti ya Shirika la habari la Wanafunzi wa Iran (ISNA): Siku ya Ijumaa jioni utawala wa Kizayuni uliilenga Hospitali ya Shahidi Salah Ghandour iliyoko katika mji wa Bint Jbeil kusini mwa Lebanon kwa mashambulizi makali  ya mizinga na kusababisha watu 9 kujeruhiwa huku wote wakiripotiwa kuwa katika hali mbaya zaidi.
Katika kivuli cha  kuwalenga kwa makusudi wafanyakazi wa afya na magari ya kubebea wagonjwa  jeshi la Kizayuni likiwa ni sehemu moja ya uchokozi wa Kizayuni unaoendeleza uchokozi  dhidi ya watu wa  Lebanon, wafanyakazi 11 wa kutoa misaada kutoka Shirika la Afya la Kiislamu wameuawa shahidi katika mashambulizi hayo ya kinyama. 

Shambulio la utawala katili wa Israeli kwenye hospitali huko Lebanon 

Habari nyingine ni kuwa, jeshi hilo katili la Kizayuni limeshambulia kwa mabomu maeneo ya makazi ya watu wa Ukanda wa  Gaza katika a kuendeleza  jinai zake za kikatili  za hivi punde.

Halikadhalika raia 13 wameuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya jeshi la Kizayuni karibu na kambi ya wakimbizi ya Nuseirat katikati mwa  Ukanda wa Gaza.
Timu za uokozi huko Ukanda wa  Gaza pia, zimetangaza kupatikana kwa miili ya Wapalestina 15 huko Khan Yunis kusini mwa Gaza kuufuatia mashambulizi makubwa ya anga ya kikatili yaliyofanywa na  jeshi la Israel.

Utawala katili wa Israel ulianzisha mauaji ya kimbari tangu Oktoba 7, 2023  kwa uungaji mkono kamili wa nchi za Magharibi na washirika wake wakuu wakiwa ni Marekani huko katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan  na matokeo yake Wapalestina zaidi ya 42,000 wameuawa shahidi na zaidi ya watu 97,000 wamejeruhiwa.

Tags