-
Human Rights Watch yakiri kuhusika utawala wa Kizayuni wa Israel na jinai za kivita
Nov 17, 2024 23:04Katika ripoti yake ya hivi karibuni zaidi, shirika la kuteteta haki za binadamu la Human Rights Watch kwa mara nyingine tena limetangaza kuwa utawala haramu wa Israel umefanya jinai za kivita dhidi ya binadamu na mauaji ya kikabila huko Gaza, kuharibu vyanzo vya maisha na kuwafanya kuwa wakimbizi mara kadhaa asilimia 90 ya wakaazi wa Gaza.
-
Msemaji wa Hizbullah auawa shahidi katika shambulio la kinyama la Israel
Nov 17, 2024 11:19Mohammad Afif, afisa wa habari wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ameuawa shahidi katika shambulio la utawala wa Kizayuni huko Ras al-Naba, Beirut mji mkuu wa Lebanon.
-
Israel yafanya mauaji mengine ya halaiki Ghaza, yawaua shahidi Wapalestina wasiopungua 96
Nov 17, 2024 09:34Wapalestina wasiopungua 96 wameuawa shahidi na wengine 60 wamejeruhiwa katika mashambulizi ya kinyama ya anga yaliyofanywa leo na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kaskazini na katikati mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Katika muda wa siku moja, jeshi la Kizayuni lafanya mashambulio 145 nchini Lebanon
Nov 17, 2024 09:11Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi 145 nchini Lebanon katika muda wa saa 24 zilizopita huku likishaidisha hujuma zake za kinyama dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu kinyume na wito wa kimataifa wa kuutaka utawala huo haramu usimamishe mashine yake ya mauaji katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Makazi ya Netanyahu yarushiwa moto, inadhaniwa ni hujuma ya wapinzani wake wa ndani
Nov 17, 2024 04:19Mapema usiku wa kuamkia leo, moto umerushwa katika makazi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, huko Caesarea, tukio lililoelezwa kuwa ni "kuongezeka kwa hatari."
-
Bunge la Yemen: Mashambulizi ya Israel dhidi ya Damascus ni jinai
Nov 16, 2024 23:51Bunge la Yemen limelaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni katika mji mkuu wa Syria, Damascus na kuitaja hujuma hiyo ya Wazayuni kuwa ni jinai.
-
Mwanahistoria wa Israel: Sasa ni wakati wa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Tel Aviv
Nov 16, 2024 22:57Katika mahojiano na gazeti la El Pais la Uhispania, mwanahistoria wa Israel, Ilan Pappé amesema kuwa "mauaji ya kimbari ya Gaza yanafanywa na utawala unaoamini kuwa umepata fursa ya kihistoria ya kuiangamiza Palestina" na amesisitiza kuwa: "Sasa ni wakati wa kuwekwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Tel Aviv.
-
Hizbullah yashambulia maeneo ya kistratijia ya utawala wa Kizayuni wa Israel
Nov 16, 2024 22:57Kituo cha Taarifa za Vita cha Hizbullah ya Lebanon kimetangaza kuwa wapiganaji wa harakati hiyo wamefanya mashambulizi ya makombora katika maeneo kadhaa ya kistratijia ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Wapalestina wengine 18 wauawa shahidi Gaza
Nov 16, 2024 11:31Wapalestina wengine 18 wameuawa shahidi katika jinai mpya iliyotekelezwa na jeshi la utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Qatar yaonya kuhusu kupigwa marufuku UNRWA
Nov 16, 2024 09:55Serikali ya Qatar imeonya kuhusiana na hatua ya kupigwa marukufu shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) na kusisitiza udharura wa kuheshimiwa haki za Wapalestina.