-
Wataalamu: Baada ya siku 150, Israel haijafikia hata lengo moja la kijeshi katika vita vya Ghaza
Mar 06, 2024 00:07Wataalamu wa masuala ya kijeshi wamesema, baada ya kupita siku 150, utawala wa Kizayuni wa Israel haujaweza kufikia malengo uliyotangaza kuwa sababu ya kuanzisha vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza, licha ya kuua maelfu ya Wapalestina, kujeruhi maelfu ya wengine, mbali na mamia ya maelfu walioachwa bila makazi pamoja na kuugeuza ukanda huo kuwa eneo la magofu.
-
Ulimwengu wa Kiislamu watakiwa ujiweke tayari kupambana vikali kwa ajili ya Palestina
Mar 06, 2024 00:06Spika wa Bunge la Uturuki Numan Kurtulmus ametoa wito kwa Ulimwengu wa Kiislamu kusimama na Palestina katika mapambano yake dhidi ya kukaliwa ardhi zake kwa mabavu na mauaji ya kimbari.
-
UNRWA yaonya: Watoto wa Gaza wanakufa polepole mbele ya macho ya walimwengu
Mar 05, 2024 03:55Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, limeonya kuhusu vifo vingi vya watoto katika Ukanda wa Gaza huku kukiwa na ukosefu mkubwa wa chakula na upatikanaji wa maji salama na huduma za matibabu katika eneo hilo.
-
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu aonya kuhusu kushadidi kwa vita vya Gaza
Mar 04, 2024 23:09Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuhusu kushadidi vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wanaoishi katika Ukanda wa Gaza.
-
Ansarullah ya Yemen: Baada ya tuliyoizamisha, tutaendelea kuzishambulia meli za Uingereza katika Bahari Nyekundu
Mar 04, 2024 05:37Yemen imeapa kuwa itaendelea kuzishambulia meli za Uingereza katika Bahari Nyekundu ili kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza, ambao wamekuwa wakiandamwa na vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa muda wa miezi mitano sasa.
-
Kimya cha taasisi za kimataifa kuhusu kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.
Mar 04, 2024 04:34Licha ya kuendelea mgogoro wa Ukanda wa Ghaza na kushadidi jinai za utawala ghasibu wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina, lakini Umoja wa Mataifa na taasisi zinazohusiana na umoja huo hadi sasa zimeshindwa kuchukua hatua mahimu katika kutetea haki za Wapalestina.
-
Waziri Mkuu wa Iraq: Iran ilikuwa pamoja nasi bega kwa bega katika vita dhidi ya Daesh (ISIS)
Mar 04, 2024 03:39Waziri Mkuu wa Iraq amesisitizia ulazima wa kutimuliwa wanajeshi wa kigeni wanaoongozwa na Marekani nchini humo na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ikiwa ni nchi jirani yenye mafungamano makubwa ya kidini na kijamii na wananchi wa Iraq, inaisaidia Baghdad katika vita dhidi ya magaidi wakiwemo wa Daesh au ISIS.
-
Kuongezeka mgawanyiko katika Baraza la Mawaziri la Vita la utawala wa Kizayuni kutokana na safari ya Gantz nchini Marekani
Mar 03, 2024 22:58Safari ya Benny Gantz, mmoja wa wajumbe wa Baraza la Mawaziri la Vita la utawala wa Kizayuni huko Marekani imekosolewa vikali na Benyamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala huo.
-
Shehbaz Sharif ateuliwa kuwa waziri mkuu wa Pakistan baada ya uchaguzi wenye utata
Mar 03, 2024 08:53Shehbaz Sharif ameteuliwa kuwa waziri mkuu wa Pakistan kwa mara ya pili, wiki tatu baada ya uchaguzi wenye utata uliopelekea kuundwa kwa serikali ya mseto.
-
Wanajihadi wa HAMAS wadhibiti ndege isiyo na rubani ya Israel
Mar 03, 2024 04:09Wanamapambano wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS wametangaza habari ya kutwaa na kudhibiti ndege isiyo na rubani ya Israel (droni), ikiwa ni kuendelea kujibu jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.