Shule zafungwa Delhi, India kutokana na uchafuzi wa hali ya hewa
https://parstoday.ir/sw/news/world-i77024-shule_zafungwa_delhi_india_kutokana_na_uchafuzi_wa_hali_ya_hewa
Shule zote katika mji mkuu wa India, New Delhi zimefungwa kutokana na hali chafu ya hewa.
(last modified 2026-03-03T12:46:59+00:00 )
Nov 17, 2021 23:26 UTC
  • Shule zafungwa Delhi, India kutokana na uchafuzi wa hali ya hewa

Shule zote katika mji mkuu wa India, New Delhi zimefungwa kutokana na hali chafu ya hewa.

Kamisheni ya Kusimamia Usafi wa Hali ya Hewa nchini India imesema taasisi zote za elimu nchini humo kuanzia jana Jumatano zitafungwa kwa muda usiojulikana, hadi taarifa mbadala itakapotolewa. 

Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu kiwango cha usafi wa hewa katika miji mikubwa duniani zinaonesha kuwa, mji mkuu wa India, New Delhi ndio wenye hewa chafu zaidi duniani.

Polisi wa trafiki aliyevaa barakoa kutokana na hali chafu ya hewa Delhi

Ripoti ya jarida la Lancet ya mwaka jana inaonesha kuwa, watu 17,500 waliaga dunia jijini Delhi kutokana na uchafuzi wa hali ya hewa mwaka juzi 2019.

Januari mwaka huu, Shirika la Afya Duniani WHO lilitangaza kuwa, watu zaidi ya milioni saba hufariki dunia kila mwaka duniani kote kutokana na uchafuzi wa hali ya hewa.