-
Misri yafuta safari ya waziri wa Brazil nchini humo kutokana na Quds
Nov 06, 2018 04:34Misri imesimamisha safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Brazil aliyetazamiwa kuitembelea nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika wiki hii, kulalamikia kitendo cha Rais Mteule wa nchi hiyo ya Amerika ya Latini kusema kuwa nchi hiyo itauhamishia ubalozi wake ulioko Israel katika mji wa Quds Tukufu.
-
Viongozi wa Kikristo mjini Quds wakosoa ubaguzi wa Netanyahu
Nov 06, 2018 04:30Wakuu wa Kanisa Katoliki katika mji wa Quds tukufu unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel wamemuandikia barua Waziri Mkuu wa utawala huo ghasibu wakikosoa misimamo yake ya kibaguzi.
-
Rais mteule wa Brazil akosolewa kwa kutaka kuuhamishia ubalozi wa nchi yake Quds
Nov 02, 2018 04:34Rais mteule wa Brazil amekosolewa vikali ndani na nje ya nchi kwa kusema kuwa nchi hiyo inatathmini mpango wa kuuhamishia ubalozi wake mjini Quds tukufu inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel kutoka Tel Aviv.
-
Wapalestina zaidi 300 wameuliwa shahidi tangu Quds itangazwe kuwa mji mkuu wa Israel
Nov 01, 2018 12:51Kituo cha Palestina cha Quds cha taaluma za masuala ya Kizayuni kimetangaza kuwa Wapalestina zaidi ya 300 wameuliwa shahidi na askari wa Israel tangu Baitul Muqaddas itangazwe kuwa mji mkuu wa utawala huo wa Kizayuni.
-
Makumi ya walowezi wa Kizayuni wavamia Msikiti wa al-Aqswa
Oct 31, 2018 04:46Makumi ya walowezi wa Kizayuni wamevamia Msikiti wa al-Aqswa wakiwa wanasaidiwa na askari wa jeshi la utawala haramu wa Israel na kufanya vitendo vya kuuvunjia heshima msikiti huo mtakatifu.
-
PLO: Hakuna amani Mashariki ya Kati bila ya kuundwa dola huru la Palestina
Oct 26, 2018 01:05Msemaji wa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa, amani haiwezi kupatikana katika eneo la Mashariki ya Kati bila ya kuundwa nchi huru ya Palestina mji mkuu wake ukiwa Quds tukufu.
-
Kuugawanya kimatumizi Msikiti mtukufu wa Al-Aqsa kwa mahali na wakati kwa lengo la kuuyahudisha
Oct 25, 2018 04:47Wazayuni wenye misimamo ya kufurutu mpaka wanaounga mkono njama za kuubomoa msikiti mtukufu wa Al-Asqa na kujenga mahali pake hekalu bandia la Kiyahudi wamependekeza mpango hatari na wa ubaguzi wa kimbari kwa madhumuni ya kupagawanya mahali hapo patakatifu.
-
'Israel inahaha mbele ya uwezo mkubwa wa kijeshi wa Hizbullah ya Lebanon'
Oct 19, 2018 21:39Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Kidemokrasia kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina amesema kuwa, utawala haramu wa Kizayuni unahaha hivi sasa kutokana na uwezo mkubwa wa kijeshi wa Hizbullah ya Lebanon na hauthubutu kuanzisha vita vingine.
-
Wapalestina 6 wauliwa shahidi na zaidi ya 190 wajeruhiwa katika Ijumaa ya "Intifadha ya Quds"
Oct 13, 2018 00:09Wapalestina wasiopungua sita wameuliwa shahidi na wengine zaidi ya 190 wamejeruhiwa katika Ijumaa ya 29 ya maandamano ya "Haki ya Kurejea" yaliyofanyika kwa kaulimbiu ya "Intifadha ya Quds" huko Ukanda wa Gaza Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Ahmad Bahar: Quds ni mji mkuu wa milele wa Palestina
Oct 06, 2018 11:56Naibu Spika wa Bunge la Palestina amesema kuwa, hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuitangaza Quds kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel haiwezi kubadilisha ukweli wa mambo kwani Quds utaendelea kubakia kuwa mji mkuu wa daima wa Palestina.