Asasi za kiraia nchini Sudan zasisitizia kuendeleza maandamano dhidi ya serikali
Asasi za kiraia nchini Sudan, zimesisitizia kuendeleza maandamano dhidi ya serikali juu ya siasa zake mbovu katika kupandisha bei ya mafuta nchini.
Taarifa iliyotolewa leo na asasi hizo imesisitiza kuwa, kamwe wananchi hawatokubaliana na maamuzi mapya ya serikali na badala yake zitaendeleza juhudi zake za kumlazimisha Rais Omar al-Bashir wa nchi hiyo aangalie upya suala hilo la kuongeza bei ya nishati hiyo muhimu.
Wakati huo huo, mamia ya wanawake wa Sudan wamemiminika mabarabarani katika mitaa ya mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum wakiitaka serikali kuheshimu matakwa ya walio wengi na kusimamisha utekelezwaji wa siasa zisizo sahihi kuhusiana na uchumi. Miji ya Atbara na Niyalah, katikati mwa mkoa wa Darfur Kusini, ni kati ya maeneo yaliyoshuhudia maandamano kulalamikia siasa za uchumi za serikali ya Sudan.
Maandamano hayo dhidi ya serikali yanazidi kushika kasi katika hali ambayo, maelfu ya raia wa taifa hilo wametaka kukomeshwa mpango wa kutekelezwa siasa za kubana matumizi sanjari na kufanyika marekebisho ya kiutawala.