Udharura wa kutoa jibu waungaji mkono wa magaidi wanaotumia silaha za kemikali
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i20446-udharura_wa_kutoa_jibu_waungaji_mkono_wa_magaidi_wanaotumia_silaha_za_kemikali
Mwakilishi wa Iran katika Shirika Linalopiga Marufuku Silaha za Kemikali (OPCW) ameeleza kuwa nchi zinazoyaunga mkono makundi ya kigaidi yanayotumia silaha za kemikali zinapasa kutoa jibu kuhusu suala hilo.
(last modified 2026-02-15T09:07:51+00:00 )
Nov 30, 2016 03:46 UTC
  • Udharura wa kutoa jibu waungaji mkono wa magaidi wanaotumia silaha za kemikali

Mwakilishi wa Iran katika Shirika Linalopiga Marufuku Silaha za Kemikali (OPCW) ameeleza kuwa nchi zinazoyaunga mkono makundi ya kigaidi yanayotumia silaha za kemikali zinapasa kutoa jibu kuhusu suala hilo.

Kongamano la 21 la Nchi Wanachama wa Mapatano ya Silaha za Kemikali  limeanza mkutano wake huko The Hague Uholanzi kwa kuhudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika Linalopiga Marufuku Silaha za Kemikali, wawakilishi wa ngazi ya juu wa nchi wanachama na taasisi zisizo za kiserikali. Akizungumza katika kongamano hilo jana huko The Hague Uholanzi, Alireza Jahangiri Mwakilishi wa Iran katika shirika la OPCW amekosoa ripoti zilizowasilishwa kuhusiana na utumiaji wa silaha za kemikali unaofanywa na makundi ya kigaidi huko Iraq na Syria yakiwemo makundi ya Daesh na Jabhatul Nusra.

Alireza Jahangiri Mwakilishi wa Iran katika Shirika la OPCW

 Jahangiri amebainisha kuwa, nchi zinazoyaunga mkono makundi ya kigaidi  ambazo zinafanikisha upatikanaji wa silaha za kemikali kwa ajili ya kutumiwa na makundi hayo dhidi ya raia wasio na hatia  zinapasa kutoa majibu kuhusu hatua zao hizo. Mwakilishi wa Iran katika Shirika Linalopiga Marufuku Silaha za Kemikali (OPCW) pia ameashiria kuwepo vilema na majeruhi wa silaha za kemikali nchini Iran wapatao laki moja  na kuongeza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa ikitoa umuhimu maalumu kwa Mapatano ya Silaha za Kemikali na kutaka kutekelezwa kikamilifu vipengee vya mapatano hayo.