-
Araqchi: Jenerali Soleimani alikuwa 'Mbunifu wa Mhimili wa Muqawama' Magharibi mwa Asia
Dec 29, 2025 08:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemsifu shahidi na kamanda wa vita dhidi ya ugaidi, Luteni Jenerali Qassim Soleimani na kumtaja kuwa "mbunifu wa Mhimili wa Muqawama" katika eneo Magharibi mwa Asia.
-
Jeshi la Iran: Tupo katika hali bora zaidi kumkabili adui
Dec 29, 2025 06:23Jeshi la Iran limeonya kwamba, hatua yoyote ya uadui kutoka kwa maadui itakabiliwa na jibu kali, huku likisisitiza juu ya utayarifu wake wa kulilinda na kulihami taifa.
-
Araqchi: Tunaunga mkono mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi ya Yemen
Dec 29, 2025 04:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi amesema kuna ulazima wa kulindwa umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala ya Yemen, huku kukiwa na ongezeko la mvutano katika maeneo ya kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Mawimbi ya kwanza ya satelaiti tatu za Iran yapokewa ardhini kwa mafanikio + VIDEO
Dec 28, 2025 23:51Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Iran ametangaza kwamba mawimbi ya kwanza ya satelaiti zote tatu zilizobuniwa na kutengenezwa ndani ya Iran zinazoitwa "Zafar 2", "Paya" na "Kowsar" zilizotumwa angani Jumapili jioni Disemba 28, 2025 yamepokewa kwa mafanikio ardhini akisisitiza kuwa, hii inathibitisha uzima wa kiufundi na utendajikazi mzuri wa satelaiti hizo za Iran baada ya kuingia kwenye obiti.
-
Satelaiti tatu za Iran zarushwa katika anga za mbali, ni hatua madhubuti ya kiteknolojia
Dec 28, 2025 09:31Satelaiti tatu za Iran zilizoundwa ndani ya nchi , ‘Paya’, ‘Zafar 2’ na ‘Kowsar’, leo zimerushwa katika anga za mbali kwa kutumia roketi ya kubeba satelaiti aina ya Soyuz kutoka kituo cha anga cha Vostochny kilichoko nchini Russia.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Qatar wajadili matukio ya kikanda hasa hali ya Yemen
Dec 28, 2025 06:59Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Qatar wamezungumza kwa njia ya simu na kubadilishana mawazo kuhusu matukio ya kikanda hususan matukio ya karibuni huko Yemene. Wamesema kuwa ipo haja ya kulindwa mamlaka ya kujitawal ya ardhi nzima ya nchi hiyo.
-
Iran: Tumejiandaa kutoa jibu chungu zaidi kwa wavamizi
Dec 28, 2025 03:17Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameonya kwamba, kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kitakabiliwa na jibu la haraka na la kuumiza zaidi, akisisitiza utayarifu wa Vikosi vya Jeshi vya nchi hii kukabiliana na maadui na vitisho vyao.
-
Iran yalaani hatua ya Israel ya kukiuka mamlaka ya kujitawala Somalia
Dec 28, 2025 00:04Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kukiukaji wazi mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi ya Somalia.
-
Ujumbe Kiongozi Muadhamu kwa Umoja wa Jumuiya za Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya; kubebwa na Iran bendera ya kukabiliana na utaratibu usio wa kiadilifu
Dec 27, 2025 07:41Katika ujumbe wake kwa mkutano wa kila mwaka wa Umoja wa Jumuiya za Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: "Taifa la Iran kwa kutumia uwezo wake linaweza kusimama na kutoa wito wa thamani za Kiislamu kwa walimwengu kwa sauti kubwa kuliko wakati mwingine wowote."
-
Ayatullah Khamenei: Mashambulizi ya Marekani na Israel yalishindwa kwa hima na ushujaa wa vijana wa Iran
Dec 27, 2025 06:18Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, amesema mashambulio makubwa ya jeshi la Marekani na mwanaharamu wake katika eneo la Magharibi mwa Asia yalishindwa kutokana na ubunifu, ushujaa na kujitolea kwa vijana wa Iran ya Kiislamu.