-
WHO: Wapalestina 22,000 wanateseka na majeraha yanayobadili maisha
Sep 13, 2024 08:14Ripoti mpya ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO imebaini kwamba kwamba takriban robo ya Wapalestina waliojeruhiwa katika vita vya mauaji ya kimbari vya Israel dhidi ya Gaza ambao ni sawa na watu 22,500 wanakabiliwa na majeraha ya kubadilisha maisha ambayo yanahitaji huduma za marekebisho sasa na kwa miaka ijayo.
-
Wafanyakazi 6 wa UN miongoni mwa watu 18 waliouliwa katika shambulio la kinyama la Israel Ghaza
Sep 12, 2024 04:10Wafanyakazi sita wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) ni miongoni mwa watu 18 waliouawa hapo jana katika shambulizi la kinyama lililofanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika skuli inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa katika Ukanda wa Ghaza ya Kati.
-
Sinwar: Kuuawa shahidi Haniya kutaongeza uthabiti wetu hadi tuifute Israel katika ardhi yetu
Sep 12, 2024 04:10Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, Yahya Sinwar amesema kuuawa shahidi mtangulizi wake Ismail Haniya na wapiganaji wengine wa Palestina kutaongeza nguvu ya Muqawama katika mapambano yake ya kuutokomeza utawala bandia wa Kizayuni wa Israel.
-
Malengo ya kimkakati ya Netanyahu kupitia mauaji ya kimbari ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza
Sep 11, 2024 22:54Utawala bandia na wa ubaguzi wa rangi wa Israel unajiandaa kwa awamu inayofuata ya vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza.
-
Wanajeshi kadhaa wa Israel waangamizwa baada ya helikopta yao kuanguka Ukanda wa Gaza
Sep 11, 2024 08:49Helikopta ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel imeanguka katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza, na kupelekea idadi kubwa ya wanajeshi wa utawala huo ghasibu kuangamia na wengine kujeruhiwa wakiwa katika operesheni ya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo..
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu: 'Kusimamishwa uchokozi wa utawala wa Kizayuni huko Gaza ni takwa la kimataifa'
Sep 11, 2024 02:35Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amekosoa kitendo cha jamii ya kimataifa cha kushindwa kusimamisha jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya raia wa kawaida wa Palestina na kusisitiza kwamba kusitishwa mauaji ya kimbari dhidi ya raia hao madhulumu huko Gaza ni takwa la kimataifa.
-
Afisa wa Hamas: Marekani inahalalisha kwa kila njia mauaji ya kimbari ya Israeli
Sep 11, 2024 02:07Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas amekosoa misimamo ya Marekani kuhusu vita vya Gaza na kusema: 'Washington inahalalisha kwa kila njia mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.'
-
Ukweli wa kushtusha wafichuliwa kuhusu UK inavyoshirikiana na Israel katika vita vya Ghaza
Sep 10, 2024 22:52Kiongozi wa zamani wa Chama cha Leba cha Uingereza Jeremy Corbyn ameikosoa vikali serikali ya nchi hiyo kwa namna inavyoshirikiana na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika kuvuruga zaidi hali ya mambo katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Israel imeua kinyama Wapalestina katika 'eneo salama' kwa mabomu mazito iliyopatiwa na Marekani
Sep 10, 2024 22:51Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel lilitumia mabomu makubwa liliyopatiwa na Marekani kushambulia "eneo salama la kibinadamu" kusini mwa Ukanda wa Ghaza, na kuzifukia familia nzima kadhaa.
-
Maandamano makubwa katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu ya kupinga vita
Sep 10, 2024 22:50Vyombo vya habari vya Israel vimetangaza kuwa, takriban watu nusu milioni katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu (Israel) wametoa wito wa kusitishwa kwa vita vya Gaza kwa kufanya maandamano dhidi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na baraza lake la mawaziri.