-
Kuendelea uungaji mkono wa jamii ya kimataifa hususan nchi za Kiislamu kwa wananchi wa Gaza
Oct 17, 2023 22:58Sambamba na kupita zaidi ya siku kumi tangu utawala wa Kizayuni wa Israel uanze kufanya jinai dhidi ya wananchi wa Gaza, himaya na uungaji mkono wa kimataifa kwa watu wa Gaza na wanamapambano wa Palestina nao unaendelea.
-
Hujuma mpya za Israel zaua shahidi Wapalestina 70 Rafah, Khan Younis
Oct 17, 2023 10:24Wapalestina wasiopungua 70 wameuawa shahidi katika mashambulizi mapya ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika miji ya Rafah na Khan Younis, kusini mwa eneo la Ukanda wa Gaza, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Uturuki kuwasilisha OIC mpango pendekezwa wa kutatua mgogoro wa Gaza
Oct 17, 2023 08:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki ametangaza kuwa atawasilisha katika kikao cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC mpango uliopendekezwa na nchi yake kwa ajili ya kutatua mgogoro wa Gaza
-
Sababu za kuakhirishwa vita vya ardhini dhidi ya Gaza
Oct 17, 2023 07:54Utawala wa Kizayuni wa Israel ulipaswa kuanzisha vita vya ardhini dhidi ya eneo la Ukanda wa Gaza kuanzia juzi, Jumapili, lakini uamuzi huo umeahirishwa.
-
Ulazima wa kuchukuliwa hatua za kuzuia jinai zinaoongezeka za Israeli huko Gaza
Oct 17, 2023 00:21Katika siku ya kumi ya uvamizi wa kijeshi wa utawala ghasibu wa Israel katika Ukanda wa Ghaza baada ya operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa, maeneo ya makazi katika ukanda huo bado yanaendelea kulengwa na mashambulizi ya utawala huo. Kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Afya ya Palestina, asilimia 66 ya wahanga wa jinai hiyo ni watoto.
-
Hamas: Nchi zinazounga mkono mashambulizi ya Israel zinahusika katika mauaji ya watoto na wanawake
Oct 17, 2023 00:17Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ilisema jana Jumatatu kuwa, nchi zinazounga mkono uvamizi wa Israel katika hujuma yake inayoendelea dhidi ya Ukanda wa Gaza unaozingirwa zinahusika katika mauaji ya watoto, wanawake na raia.
-
Mwandishi wa Israel: Wazayuni 1,815 wamengamizwa na Hamas
Oct 17, 2023 00:10Yossi Milman mwandishi habari mtajika Mzayuni ameandika katika ukurasa wake wa X, Twitter ya zamani, kwamba hadi sasa Wazayuni 1,815 wameuawa katika mashambulizi ya wanamapambano wa Hamas.
-
Idadi ya mashahidi wa Palestina huko Gaza yafikia 2700
Oct 16, 2023 10:19Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza ongezeko la idadi ya mashahidi na waliojeruhiwa katika hujuma ya jeshi la utawala wa Kizayuni katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza.
-
Pengo la wazi katika misimamo ya wananchi na madola yenye nguvu duniani kuhusu vita vya Gaza
Oct 16, 2023 04:28Siku kumi zimepita tangu kuanza vita vya pande zote vya utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Ghaza, ambapo huku wananchi wa mataifa mbalimbali wakilaani jinai za utawala huo unaoukalia kwa mabavu Quds Tukufu, mabeberu wa dunia bado wanaendelea ima kuunga mkono utawala huo ghasibu au kunyamazia kimya jinai zake za kivita.
-
WHO: Israel imeangamiza familia zote za Wapalestina katika kampeni ya mashambulizi Ghaza
Oct 15, 2023 23:00Shirika la Afya Duniani (WHO) limeeleza kuwa kumekuwa na maangamizi ya familia zote za Wapalestina katika Ukanda wa Gaza kutokana na mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya eneo hilo la pwani lililozingirwa katika siku chache zilizopita.