-
Kwa nini Hizbullah inapinga makubaliano ya serikali ya Lebanon na Israel?
Jun 29, 2026 09:05Sheikh Naim Qassim, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, na baadhi ya wabunge wa Hizbullah wamekosoa na kupinga vikali mazungumzo yanayodaiwa kufikiwa kati ya serikali ya Lebanon na utawala haramu wa Israel.
-
Taasisi ya Hind Rajab yawasilisha mashtaka Wizara ya Sheria ya Marekani dhidi ya Ben-Gvir
Jun 29, 2026 03:40Taasisi ya Hind Rajab (HRF) imewasilisha malalamiko kwa Wizara ya Sheria ya Marekani (DoJ), ikitaka kukamatwa na kushtakiwa anayeitwa waziri wa usalama wa taifa wa utawala wa Israel, Itamar Ben-Gvir kwa tuhuma za kutenda jinai.
-
Ripoti: Gaza inatafuta maiti 8,500 za mauaji ya kimbari ya Israel chini ya vifusi kwa kutumia chombo kimoja
Jun 29, 2026 03:34Ripoti kutoka Ukanda wa Gaza zinasema kuwa chombo kimoja cha kuchimba vifusi (excavator) tu kinatumiwa kutafuta karibu miili ya watu 8,500 na mabaki yaliyo chini ya vifusi vya nyumba zilizoharibiwa na jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya kimbari katika eneo hilo.
-
Maandamano kote Lebanon kupinga makubaliano yanayoungwa mkono na Marekani na Israel
Jun 27, 2026 11:04Maelfu ya wananchi wa Lebanon wamejitokeza mitaani katika miji na maeneo mbalimbali kupinga “makubaliano” yanayoungwa mkono na Marekani kati ya Lebanon na utawala wa Israel, huku wakiyataja kuwa tishio kwa mamlaka ya taifa lao.
-
Kiongozi wa Hizbullah: Israel italazimika kuondoka Lebanon “ikiwa imedhalilika”
Jun 27, 2026 02:59Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sheikh Naim Qassem, amesema kuwa Israel italazimika kuondoka bila masharti katika kila sehemu ya ardhi ya Lebanon, ikiwa “imeshindwa na kudhalilika.”
-
Ansarullah yatishia kushambnulia vituo vyovyote vya Israel katika eneo la Somaliland
Jun 26, 2026 11:20Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Abdul-Malik al-Houthi, ameapa kwamba atashambulia uwepo wowote wa Israel katika eneo lililojitenga na Somalia la Somaliland kwa njia zote zinazowezekana, akisisitiza kwamba Yemen "haitakaa kimya mbele ya uwepo wowote wa Israel huko Somaliland, na haitawasubiri waoga."
-
Qalibaf: Mpangilio mpya wa Kiislamu uundwe baada ya Marekani na Israel kudhalilishwa katika vita dhidi ya Iran
Jun 25, 2026 04:27Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa wito kwa mataifa ya Asia Magharibi na ulimwengu wa Kiislamu kuanzisha mpangilio mpya wa kikanda unaotegemea uwezo, rasilimali na watu wa mataifa hayo, akisisitiza kwamba “chanzo cha misiba yote ni utawala wa Kizayuni.”
-
Hizbullah: Israel haiwezi kamwe kufikia malengo yake katika medani ya vita
Jun 25, 2026 04:25Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon, ameashiria "kugonga mwamba wa mradi wa Israel," na kusisitiza kwamba, utawala huu hautaweza kamwe kufikia malengo yake katika medani ya vita.
-
WHO: Hakuna hospitali yoyote Gaza inayofanya kazi kwa uwezo wake kamili
Jun 25, 2026 04:14Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kwamba hakuna hospitali yoyote katika Ukanda wa Gaza inayofanya kazi kwa uwezo wake kamili kwa sasa, na kwamba, uhaba mkubwa wa vifaa vya matibabu na mafuta umeweka utoaji wa huduma za afya katika hatari kubwa.
-
Tasu'a ya Imam Hussein (AS) yaunganisha mamilioni ya Wairani, waapa kuendeleza mapambano
Jun 24, 2026 04:23Wairani katika mji mkuu Tehran, majiji, miji na vijiji vyote nchini usiku wa kuamkia leo walikusanyika misikitini na katika vituo vya kidini na barabarani katika marasimu ya kuadhimisha Tasu'a, siku ya tisa ya mwezi Muharram, kuelekea kwenye Siku ya Ashura ya kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein (AS), mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW).