Wabunge Sudan warejesha nafasi ya waziri mkuu
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i22342-wabunge_sudan_warejesha_nafasi_ya_waziri_mkuu
Wabunge nchini Sudan wamepiga kura ya kubadilisha katiba ili nafasi ya waziri mkuu irejeshwa tena nchini humo baada ya miongo miwili.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Dec 29, 2016 03:49 UTC
  • Wabunge Sudan warejesha nafasi ya waziri mkuu

Wabunge nchini Sudan wamepiga kura ya kubadilisha katiba ili nafasi ya waziri mkuu irejeshwa tena nchini humo baada ya miongo miwili.

Rais Omar al Bashir alifuta nafasi ya waziri mkuu baada ya kunyakua madaraka mwaka 1989.

Siku ya Jumatano, wabunge 387 kati ya 425 walipiga kura ya kuunga mkono marekebisho hayo ya katiba ya kuruhusu waziri mkuu ateuliwe na rais na awe na nguvu za utendaji nchini.

Pamoja na hayo, jukumu la kuunda serikali au kuwafuta kazi mawaziri litabakia mikononi mwa rais.

Maandamano dhidi ya utawala wa Bashir nchini Sudan

Hatua hiyo inaonekana kuwa sehemu ya marekebisho yaliyopendekezwa katika mazugumzo ya kitaifa baina ya serikali na baadhi ya makundi ya upinzani. Mazungumzo hayo yalianza mwezi Oktoba kwa lengo la kusuluhisha matatizo ya kisiasa na kiuchumi  na pia kumaliza uasi katika maeneo ya mipakani nchini humo.

Waziri mkuu mpya wa Sudan atakuwa na jukumu la kusimamia serikali hadi wakati wa kufanyika uchaguzi wa bunge mwaka 2020. Tayari Rais Bashir ametangaza kuwa, ataachia madaraka ifikapo mwaka 2020 kwani katiba ya Sudan haitomruhusu kuendelea kutawala.