Jeshi la Sudan lakanusha kushambulia waasi katika jimbo la Blue Nile
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i34481-jeshi_la_sudan_lakanusha_kushambulia_waasi_katika_jimbo_la_blue_nile
Jeshi la Sudan limekanusha kushambulia eneo la waasi katika jimbo la Blue Nile.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Sep 17, 2017 09:25 UTC
  • Jeshi la Sudan lakanusha kushambulia waasi katika jimbo la Blue Nile

Jeshi la Sudan limekanusha kushambulia eneo la waasi katika jimbo la Blue Nile.

Jeshi la Sudan limetoa taarifa na kusisitiza ahadi zake za kusitisha mapigano katika maeneo yote ya migogoro, na kukanusha madai ya waasi kwamba jeshi hilo lilishambulia eneo lao katika jimbo la Blue Nile.

Siku ya Ijumaa, kundi la waasi la Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Sudan (SPLM) – Eneo la Kaskazini- lilishutumu jeshi la serikali ya Khartoum kuwa limeshambulia ngome yake katika jimbo hilo.

Rais Bashir wa Sudan

Msemaji wa jeshi la Sudan Ahmed Khalifa Al-Shami ameeleza kuwa, jeshi la Sudan linasisitiza tena ahadi zake za kusitisha mapigano dhidi ya waasi.

Amesema shutuma ya waasi ina kusudi la kuharibu ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Sudan huko Washington.

Mwezi Julai, Rais wa Sudan Omar al-Bashir alitangaza kusimamisha mapigano katika maeneo yote ya migogoro kwa miezi mitatu hadi Oktoba mwaka huu.