Kenya yatakiwa kukata uhusiano na utawala pandikizi wa Israel +SAUTI
Jun 07, 2018 14:58 UTC
Wanaharakati wa vuguvugu la Muungano wa Kenya na Palestina wameapa kuishinikiza serikali kusitisha uhusiano na serikali ya kidhalimu ya Israel na washirika wake wa karibu kama vile Marekani, baada ya madola hayo kuendeleza hujuma za wazi dhidi ya Wapalestina na kuikalia ardhi yao kwa mabavu.
Wanaharakti hao wameyasema hayo kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds, ambayo huadhimishwa kila Ijumaa ya mwisho ya mwezi wa Ramadhani ;ambapo mwaka huu pia itaadhimishwa duniani kote sawa na tarehe 8 Juni.
Tags