Utafiti: Jinai zimeongezeka katika miji mikubwa Marekani
https://parstoday.ir/sw/news/world-i12361-utafiti_jinai_zimeongezeka_katika_miji_mikubwa_marekani
Utafiti mpya umefichua kuwa uhalifu na jinai za kutisha zimeongeza kwa kiasi kikubwa katika miji mikubwa ya Marekani.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jul 31, 2016 23:25 UTC
  • Utafiti: Jinai zimeongezeka katika miji mikubwa Marekani

Utafiti mpya umefichua kuwa uhalifu na jinai za kutisha zimeongeza kwa kiasi kikubwa katika miji mikubwa ya Marekani.

Utafiti huo uliofanywa na shirika la Major Cities Chiefs Association umeonyesha kuwa, kuna mauaji 307 zaidi yaliyofanyika katika miji mikubwa nchini humo katika kipindi cha miezi sita ya kwanza ya mwaka huu 2016, ikilinganishwa na mauaji yaliyofanyika katika muda kama huo mwaka jana 2015.

Silaha zinazotumiwa kutekeleza jinai za kutisha Marekani

Uchunguzi wa shirika hilo umebainisha kuwa, kuna visa 2,000 vya uhalifu wa kutisha, 1,000 vya wizi wa mabavu na kesi 600 za ufyatuaji risasi ovyo zilizoripotiwa katika muda huo, ambazo ni maradufu na kesi zilizoripotiwa katika kipindi cha miezi sita ya kwanza ya mwaka jana.

Visa vingine vinavyosemekana kuongezeka katika muda huo ni mauaji ya kifamilia na ubakaji na haswa katika miji ya Chicago, Las Vegas na Orlando.

Mauaji ya Orlando jimbo la Florida, Marekani mwezi Juni 2016

Itakumbukwa kuwa, mwezi uliopita, watu zaidi ya 50 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika ufyatuaji wa risasi uliotokea katika klabu ya masenge katika mji wa Orlando jimbo la Florida nchini Marekani.