Ghana ni kituo kinachoongoza kwa bidhaa za Iran zinazouzwa barani Afrika
Msemaji wa Kamisheni ya Ustawi wa Biashara ya Chama cha Viwanda, Madini na Biashara cha Iran ametangaza kuwa, Ghana ni kituo cha kwanza kinachoongoza kwa bidhaa za Iran zinazopelekwa barani Afrika.

Latifi ameongeza kuwa kiwango hicho ni punguo la 33% katika uzito wa bidhaa na 53% katika thamani yake ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita.
Msemaji wa Kamisheni ya Ustawi wa Biashara ya Chama cha Viwanda, Madini na Biashara cha Iran amesema kuhusu vituo zinakopelekwa bidhaa za Iran katika bara la Afrika kwamba, Ghana ni kituo kilichoongoza kwa mauzo ya bidhaa za Iran katika kipindi hicho kwa ununuzi wa bidhaa zenye thamani ya dola milioni 116.3, ikifuatiwa na Afrika Kusini iliyonunua bidhaa zenye thamani ya dola milioni 89. 5, Tanzania dola milioni 61.4, Nigeria dola milioni 46.5, Msumbiji dola milioni 40, Kenya dola milioni 28.3, Somalia dola milioni 16.5, Sudan dola milioni 7.1, Libya dola milioni 5.5, Djibouti dola milioni 5.1, Algeria dola milioni 4.9, Kongo dola milioni 3.4 na Cote d'Ivoire dola milioni 3.4.../