Somalia yamtimua balozi wa Ethiopia kutokana na mgogoro wa mkataba wa bandari ya Somaliland
Somalia imetangaza kumfukuza balozi wa Ethiopia nchini humo huku kukiwa na mvutano unaoongezeka kuhusu mzozo wa makubaliano ya bandari kati ya Ethiopia na eneo lililojitenga la Somaliland.
Mzozo baina ya nchi mbili uliibuka baada ya Ethiopia isiyo na bandari kusaini hati ya makubaliano mnamo Januari 1 na eneo la Somaliland ya kukodishwa kilomita 20 (maili 12) za ukanda wa pwani ya eneo hilo.
Chini ya mpango huo, ukanda huo ulioko karibu na bandari ya Berbera, kwenye Ghuba ya Aden, utatumiwa na Ethiopia kwa miaka 50 kwa madhumuni ya kijeshi na kibiashara.
Ethiopia ilisema inataka kuanzisha kituo cha jeshi la wanamaji katika ukanda huo wa pwani ya eneo la Somaliland, mkabala wa uwezekano wa kuitambua Somaliland kama nchi na hivyo kuibua ghadhabu na hasira za Somalia - ambayo iliituhumu Ethiopia kuwa inajaribu kunyakua sehemu ya eneo lake - na kuhofia kuwa makubaliano hayo yanaweza kuyumbisha zaidi amani na uthabiti wa eneo la Pembe ya Afrika..../