Utekaji nyara watu nchini CAR waongezeka na kuogofya raia
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i11734-utekaji_nyara_watu_nchini_car_waongezeka_na_kuogofya_raia
Asasi za kiraia nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati zimeonyesha wasi wasi wake kufuatia zaidi ya watu 300 kutekwa nyara na wabeba silaha nchini humo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jul 22, 2016 03:09 UTC
  • Utekaji nyara watu nchini CAR waongezeka na kuogofya raia

Asasi za kiraia nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati zimeonyesha wasi wasi wake kufuatia zaidi ya watu 300 kutekwa nyara na wabeba silaha nchini humo.

Taasisi ya Invisible Children na The Resolve kwa pamoja zilitangaza jana kwamba, kwa kipindi cha miezi sita ya mwaka huu wa 2016, jumla ya watu 344 wakiwemo watoto 65 wametekwa nyara na waasi wa Kikristo wa Anti-Balaka. Kwa mujibu wa taasisi hizo, idadi ya watu ambao wametekwa nyara nchini humo tangu mwaka 2010, haina mfano wake.

Wanamgambo wa Kikristo wa Anti-Balaka

 

Kadhalika taasisi hizo zimetangaza kuwa, hadi sasa baadhi ya watu miongoni mwa idadi hiyo  bado wanaendelea kushikiliwa na wanachama wa kundi hilo. Kwa upande wake Sean Poole mkuu wa taasisi ya kimataifa ya watoto ameitaka jamii ya kimataiafa kusaidia kuwalinda raia kutokana na hujuma za makundi ya waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati. Nchi hiyo ilitumbukia katika machafuko mwaka 2013 baada ya makundi ya waasi kumfurusha aliyekuwa raia wa nchi hiyo François Bozizé.