Hali ya kibinadamu yazidi kuzorota katika Jamhuri ya Afrika ya Kati
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i26590-hali_ya_kibinadamu_yazidi_kuzorota_katika_jamhuri_ya_afrika_ya_kati
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa hali ya kibinadamu imeendelea kuwa mbaya katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Mar 19, 2017 12:55 UTC
  • Hali ya kibinadamu yazidi kuzorota katika Jamhuri ya Afrika ya Kati

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa hali ya kibinadamu imeendelea kuwa mbaya katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stéphane Dujarric ameyasema hayo mjini New York, Marekani na kuongeza kuwa, zaidi ya nusu ya jamii yote ya watu wa nchi hiyo wanahitaji misaada ya kibinadamu. Amesema kuwa, machafuko yaliyoshika kasi sambamba na ongezeko la vita katika maeneo tofauti ya nchi hiyo vimewalazimisha zaidi ya watu laki moja kuyakimbia makazi yao katika kipindi cha miezi kadhaa ya hivi karibuni.

Magaidi wa Kikristo wa Anti-Balaka nchini CAR

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amefafanua kuwa, licha ya kuongezeka idadi ya wakimbizi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, lakini kiwango cha misaada ya kibinadamu ambayo imekuwa kitolewa nchini humo kimeendelea kupungua tangu mwaka 2014. Machafuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati yaliongezeka zaidi baada ya wanachama wa kundi la Seleka kumuondoa madarakani François Bozizé, rais wa zamani wa nchi hiyo hapo mwaka 2013.

Wanamgambo wabeba silaha wa Seleka ambao nao wanatajwa kuhusika na machafuko

Serikali ya sasa inayoongozwa na Rais Faustin-Archange Touadéra imeshindwa kudhibiti maeneo yote ya nchi hiyo ya katikati mwa Afrika kutoka mikononi mwa wanamgambo wanaobeba silaha.