-
IRGC: Iran haiogopi vitisho na haitakubali kutawaliwa na Marekani
Jan 06, 2026 23:27Naibu Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi, amesema kuwa Iran haiogopi vitishio vya maadui na kamwe haitakubali kutawaliwa na Marekani. Ametoa kauli hiyo kujibu vitisho vilivyotolewa hivi karibuni na Rais wa Marekani Donald Trump.
-
Qalibaf: Israel ilibembeleza kusitisha mapigano wakati wa vita vya siku 12
Jan 06, 2026 08:41Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa: Katika siku chache za mwisho za vita vya siku 12, utawala wa Kizayuni uliomba kwa kubembeleza kusitisha mapigano na ukweli huo unaonesha nguvu ya Muqawama wa taifa la Iran mbele ya wavamizi.
-
Baqaei: Vikosi vya Iran viko macho kukabiliana na vitisho vyovyote vya adui
Jan 06, 2026 08:41Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje amesema kuhusu mazingira yaliyozushwa ya kuonesha kuna uwezekano wa kurudiwa uchokozi wa kijeshi dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa: Kilicho muhimu na kinachotuhusu sisi ni kuimarisha nguvu zetu na kuwa macho zaidi kulihami taifa la Iran.
-
Iran, Cuba, Brazil zataka kuheshimwa sheria za kimataifa
Jan 06, 2026 03:21Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Cuba na Brazil wamesisitiza udharura wa kuwepo ushirikiano wa karibu na uratibu miongoni mwa nchi zinazostawi katika majukwaa ya kimataifa, ili kukabiliana na mfumo wa ubeberu; na kuunga mkono sheria za kimataifa na kanuni za Hati ya Umoja wa Mataifa.
-
Iran yakanusha uvumi wa vyombo vya habari vya Magharibi kuhusu mazungumzo na Marekani
Jan 06, 2026 00:06Naibu wa Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha uvunii unaoneshwa na vyombo vya habari vya Magharibi kwamba Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alifanya mkutano maalumu na waandishi wa habari siku ya Alkhamisi na kuongeza kuwa, inavyoonekana ni kwamba baadhi ya duru za Magharibi zinapenda sana kupata kisingizio cha kusema uongo na kuchochea chuki katika kila jambo.
-
Kukariri Rais wa Marekani kauli za uingiliaji kati; Je, Trump anawajali sana watu wa Iran?
Jan 05, 2026 08:27Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena amekariri kauli zake za uingiliaji kati dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kufuatia matukio ya hivi karibuni hapa nchini.
-
Iran: Marekani lazima imwachie huru Rais iliyemteka nyara wa Venezuela
Jan 05, 2026 08:04Iran, kwa mara nyingine tena, imekosoa kitendo cha Marekani cha kumteka nyara Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro na mkewe, Cilia Flore, na kueleza kuwa waliotekwa nyara lazima waachiwe huru kama inavyosisitizwa na maafisa na wananchi wa Venezuela.
-
Qalibaf: Waandamanaji wasikilizwe, vibaraka wa mataifa ya kigeni watashughulikiwa
Jan 05, 2026 07:53Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kwamba maandamano ya watu lazima yasikilizwe, huku akionya kwamba watu binafsi wanaohusishwa na mashirika ya ujasusi ya kigeni wanaotaka kuteka nyara maandamano ya amani ya wananchi na kuyageuza kuwa ghasia, lazima washughulikiwe kivyao.
-
Mtaalamu wa Russia: Mkataba wa ushirikiano wa kimkakati kati ya Iran na Russia; hatua muhimu ya 2025
Jan 05, 2026 04:15Igor Matveev, profesa na mtaalamu wa masuala ya siasa wa nchini Russia ameutaja Mkataba Kamili wa Kimkakati uliosainiwa kati ya Iran na Russia mwanzoni mwa mwaka jana kuwa hatua muhimu katika uhusiano kati ya mataifa haya mawili.
-
Kamanda: Baada ya kushindwa vita vya Juni, US na Israel zinaendesha 'vita laini' kuvuruga utulivu Iran
Jan 04, 2026 23:47Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel zinaendesha "vita laini" ili kuvuruga uthabiti na utulivu nchini likiwa ni jaribio la kufidia kushindwa kwao katika vita vya siku 12 vya mwezi Juni zilivyoanzisha dhidi ya Iran.