-
Wabunge 150 wa Iran walaani chokochoko za Marekani nchini Venezuela
Dec 24, 2025 08:01Kundi la wabunge 150 wa Iran limeilaani vikali Marekani kwa chokochoko zake huko Venezuala na kuzuia meli za mafuta katika Bahari ya Karibi, likisema kuwa vitendo hivyo vya Washington ni uharamia wa baharini na ni tishio kwa utulivu na usalama wa ukanda huo.
-
Iran, Russia na China Zaungana katika Kupinga Snapback
Dec 24, 2025 07:02Wawakilishi wa Iran, Russia na China katika Umoja wa Mataifa wamesisitiza, katika mkutano wa Baraza la Usalama la umoja huo, kwamba madai ya Marekani pamoja na Uingereza na Ufaransa, hayakuwa halali kuhusu kurejeshwa mara moja na bila masharti vikwazo vya UN dhidi ya Jamhuri ya Kislamu maarufu kama snapback.
-
Mwakilishi wa Iran UN: Baada ya Oktoba 2025, Azimio 2231 halikuwa tena na itibari ya kisheria
Dec 24, 2025 03:17Mwakilishi wa Iran katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa cha kujadili Azimio 2231 amesema, Jamhuri ya Kiislamu inakubaliana na misimamo ya Russia na China ya kupinga kuitishwa kwa kikao hicho. Azimio 2231 lina kifungu kinachoeleza bayana kwamba muda wake wa kumalizika ni Oktoba 2025, na baada ya hapo hakutakuwa tena na msingi wa kisheria wa kuendelea majukumu ya azimio hilo.
-
Araqchi na Abdul Ati wakubaliana kuimarishwa uhusiano wa Iran na Misri
Dec 23, 2025 23:28Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Misri wamekubaliana kwa njia ya simu kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya Tehran na Cairo na matukio muhimu ya kieneo na kimataifa.
-
"Uwezo wa makombora ya Iran umeimarika, tayari kukabili adui"
Dec 23, 2025 23:10Msemaji wa Jeshi la Iran amesema kwamba, uwezo wa vikosi vya majini, ardhini, na makombora vya Jamhuri ya Kiislamu viko tayari kikamilifu kukabiliana na senario yoyote tarajiwa ya adui, akisisitiza kwamba Tehran bado haijatumia nguvu yake halisi ya makombora.
-
Utayari wa Iran wa kuanzisha mtandao wa nchi za Kiislamu wa bioteknolojia na kuimarisha usalama wa chakula
Dec 23, 2025 23:08Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Bioteknolojia ya Kilimo ya Iran ametangaza utayari wa kuanzisha mtandao wa pamoja wa ushirikiano wa kisayansi na utafiti na nchi za Kiislamu katika sekta ya usalama wa chakula.
-
Rais Pezeshkian awasilisha rasimu ya bajeti katika Bunge la Iran
Dec 23, 2025 10:03Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amewasilisha rasimu ya bajeti ya mwaka ujao wa kifedha wa Iran (kuanzia Machi 21, 2026) katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran).
-
Meja Jenerali Hatami: Tunafuatilia kwa karibu nyendo za adui
Dec 22, 2025 23:46Kamanda Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, tunafuatilia kwa karibu hatari na nyendo kwa umakini mkubwa.
-
Mtafiti mwanamke wa Kiirani ashinda tuzo ya utafiti ya COMSTECH ya mwaka 2025
Dec 22, 2025 23:45Mwanamke mtafiti Muirani amechaguliwa kuwa mmoja wa wapokeaji wa Mpango wa Tuzo ya Utafiti kwa Watafiti Vijana Wanawake wa COMSTECH kwa mwaka wa 2025.
-
Baqaei: Uwezo wa kujihami wa nchi si wa kujadiliwa; Vikosi vya ulinzi vimejiandaa kikamilifu kulilinda taifa
Dec 22, 2025 07:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa uwezo wa kiulinzi wa nchi hii kimsingi umeratibiwa kwa lengo la kuzuia mashambulizi yoyote ya wavamizi na si suala la kujadiliwa.