-
Hamas: Usitishaji mapigano lazima uhusishe kuondoka kikamilifu Israel Ukanda wa Gaza
Aug 16, 2024 04:25Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) kwa mara nyingine tena imesisitiza kuwa makubaliano yoyote na Israel lazima yahakikishe usitishaji kamili wa vita huko Gaza, kuondoka kikamili majeshi ya Israel katika eneo hilo na makubaliano ya kubadilishana wafungwa.
-
Israel yapata hasara ya dola bilioni 67 kutokana na vita vya Gaza
Aug 16, 2024 04:06Wachumi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamefichua hasara kubwa za kiuchumi za vita vya Gaza kwa utawala huo na kusema, uchumi wa Israel unakabiliwa na mgogoro usioweza kudhibitiwa.
-
Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine wataka kukomeshwa vita Gaza
Aug 16, 2024 00:53Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kuongezeka watu wanaouawa huko Gaza kunatisha na hivyo ametoa mwito wa kukomeshwa mara moja ukatili huo.
-
Israel inashinikiza ICC ifute waranti wa kukamatwa Netanyahu
Aug 15, 2024 04:13Utawala wa Kizayuni umeripotiwa kushadidisha 'mashinikizo ya kidiplomasia' dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ambayo inataka kutolewa waranti wa kukamatwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu na waziri wa vita wa utawala huo haramu, Yoav Gallant, kwa sababu ya kuhusika na uhalifu wa kivita.
-
Hali ya kutisha ya zama za mwisho huko Gaza
Aug 15, 2024 01:05Huku nchi za Magharibi zikiunga mkono jinai zinazoongezeka kila siku za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina hasa katika kuwalazimisha watu wa Gaza kuyahama makazi yao, weledi wa mambo wanasema wigo wa jinai hizo unaweza kuzikumba nchi hizo pia baada ya muda usio mrefu.
-
Bin Salman ahofia kuuawa kwa kufuatilia mpango wa kuanzishwa uhusiano rasmi kati ya Saudia na Israel
Aug 15, 2024 00:15Mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman ameripotiwa kuwa anahofia "kuuawa" kwa sababu ya juhudi zake za kutaka kuhakikisha ufalme huo unaanzisha uhusiano rasmi na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Muqawama Iraq: Jibu la Iran dhidi ya Israel litakuwa la nguvu
Aug 14, 2024 23:16Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya al-Nujabaa ya Iraq amesema jibu tarajiwa la Iran kwa mauaji ya kigaidi yaliyofanywa mwezi uliopita na utawala wa Kizayuni dhidi ya Ismail Haniyah, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS litakuwa la nguvu, lenye taathira na la kimahesabu.
-
HAMAS: Hatutashiriki mazungumzo ya usitishaji vita Doha
Aug 14, 2024 23:15Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema wawakilishi wa harakati hiyo ya muqawama hawatashiriki mazungumzo ya leo ya usitishaji vita yanayotazamiwa kufanyika Doha, mji mkuu wa Qatar.
-
Kikao cha Baraza la Usalama kuhusu vita vya Ghaza; makabiliano ya Marekani na Jamii ya Kimataifa
Aug 14, 2024 07:45Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa cha kujadili shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya Skuli ya Al-Tabeen katika Ukanda wa Ghaza kilifanyika siku ya Jumanne ambapo akthari ya wanachama wa Baraza hilo walilaani jinai ya utawala huo na kusisitiza juu ya ulazima wa kusitishwa vita mara moja huko Ghaza.
-
Sinwar: Tuko tayari kufanya mazungumzo iwapo vita vya Gaza vitasitishwa
Aug 14, 2024 04:11Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema kuwa kushiriki kwao katika mazungumzo ya Doha kunategemea na kusimamishwa vita katika Ukanda wa Gaza.