-
Hatua kwa hatua kuelekea Siku ya Kimataifa ya Quds; Marekani mshirika wa jinai za Israel dhidi ya Wapalestina
May 26, 2018 22:02Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo ni siku ya kupazwa duniani sauti ya kudhulumiwa taifa la Palestina na kuchukizwa ulimwengu na utawala katili wa Israel unaoua watoto wadogo, inawadia.
-
Kukivunja kabisa Kibla cha Kwanza cha Waislamu; hatua ya baadaye ya Trump
May 24, 2018 22:47Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, vitendo vya balozi wa Marekani vinaonesha jinsi nchi yake inavyoshirikiana na utawala wa Kizayuni wa Israel katika kuyavunjia heshima matukufu ya taifa la Palestina na ya umma mzima wa Kiarabu na wa Kiislamu.
-
Wananchi wa Morocco waandamana kulaani kuhamishiwa Quds ubalozi wa Marekani
May 21, 2018 03:27Makumi ya maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano katika mji wa Dār al-Bayḍā (Casablanca) kulaani hatua ya Marekani ya kuuhamishia Quds ubalozi wake uliokuweko Tel Aviv, mji mkuu wa utawala pandikizi wa Israel.
-
Walowezi wa Kizayuni wauhujumu Msikiti wa al Aqsa mjini Quds
May 20, 2018 22:03Walowezi zaidi ya 300 wa Kizayuni wameuhujumu Msikiti wa al Aqsa ulioko katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
HAMAS: Kuvamiwa msikiti wa Al Aqsa na walowezi wa Kizayuni kumefanywa kwa uungaji mkono wa Marekani
May 13, 2018 22:36Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, uvamizi uliofanywa walowezi wa Kizayuni katika msikiti wa Al Aqsa hapo jana ni namna fulani ya utoaji vitisho unaofanywa na utawala wa Kizayuni kwa uungaji mkono wa Marekani.
-
Kususiwa sherehe za ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Quds
May 13, 2018 06:05Zaidi ya nusu ya viongozi wa kigeni walioalikwa kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Quds, wamekataa kushiriki sherehe hizo.
-
Waisraeli wajiunga na Wapalestina katika maandamano dhidi ya US
May 13, 2018 03:16Mamia ya Waisraeli wamejiunga na Wapalestina katika maandamano ya kupinga hatua ya kiuhasama ya Marekani ya kuuhamishia ubalozi wake katika mji wa Quds Tukufu, kutoka Tel Aviv.
-
Mataifa ya Kiislamu yaandamana kupinga US kuuhamishia ubalozi wake Quds
May 12, 2018 02:54Maelfu ya watu wameshiriki maandamano ya kupinga hatua ya kiuhasama ya Marekani ya kuuhamishia ubalozi wake katika mji wa Quds Tukufu, kutoka Tel Aviv.
-
Kuchukua wigo mpana zaidi malalamiko ya Wapalestina dhidi ya njama za Trump huko Beitul-Muqaddas
May 10, 2018 07:21Ripoti mbalimbali kutoka Palestina zinaonyesha juu ya kushadidi upinzani na malalamiko ya vyama na makundi mbalimbali ya Kipalestina dhidi ya uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya mji wa Beitul-Muqaddas unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
-
Umoja wa Mataifa: Tunapinga Marekani kuhamishia ubalozi wake Beitul-Muqadas
May 09, 2018 09:47Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kwa mara nyingine tena upinzani wa taasisi hiyo kwa uamuzi wa Marekani wa kutaka kuhamishia ubalozi wake katika mji wa Beitul-Muqaddas huko Palestina inayokkaliwa kwa mabavu.