Watu 49 waghariki katika ajali ya boti mtoni kaskazini mwa Kongo DR
Watu 49 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya boti kuzama mtoni kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Richard Mboyo Iluka, Naibu Gavana wa Mkoa wa Tshuapa ameiambia Idhaa ya Radio Top Congo kwamba, ajali hiyo ilitokea Jumatano, ambapo boti hiyo dhaifu ilizama ikiwa na makumi ya abiria.
Ameongeza kuwa, watu wengine 49 wamenusurika katika ajali hiyo iliyotokea jioni ya Jumatano iliyopita.
Ajali za boti zimekuwa zikiripotiwa mara kwa mara DRC, na sababu kuu ya ajali hizo ni boti kujaza watu kupita kiasi na ubovu wa boti zenyewe.
Aghalabu ya wananchi wa Kongo DR, nchi yenye misitu mingi inayoyahifadhi makundi ya waasi, hulazimika kutumia usafiri wa boti kwenye mito, katika safari za masafa marefu.