Imamu wa Msikiti wa Al-Aqsa: Kauli ya waziri wa Israel dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa ni hatarishi
Imamu wa Msikiti wa Al-Aqsa Sheikh Ikrima Sabri amesema, kauli aliyotoa hivi karibuni waziri wa usalama wa ndani wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa ni hatarishi.
Sheikh Sabri amesema, mipango inayodaiwa na kufuatiliwa na Ben Gvir imefeli na kugonga mwamba na akatamka bayana: "tunasisitiza kuwa Msikiti wa Al-Aqsa ni wa Waislamu na tunatoa indhari dhidi ya kuukaribia".
Katika mahojiano hayo na Al Jazeera Imamu na Khatibu wa Msikiti wa Al-Aqsa amesema, miradi inayozungumziwa na utawala wa Kizayuni ni mipango hewa na ya udhanifu tu na kwamba Msikiti wa Al-Aqsa utabaki kuwa Msikiti wa Al-Aqsa; na akaongeza kuwa: mipango yao ni hewa na ya udhanifu; na baraza la mawaziri la Israel linabeba dhima kamili ya kitakachotokea dhidi ya msikiti huo.