Waislamu Ufaransa watahadharishwa kuhusu ongezeko la mashambulizi ya kigaidi
https://parstoday.ir/sw/news/world-i31284-waislamu_ufaransa_watahadharishwa_kuhusu_ongezeko_la_mashambulizi_ya_kigaidi
Viongozi wa makundi na jumuiya mbalimbali za Kiislamu nchini Ufaransa wamewatahadharisha wafuasi wa dini hiyo kuhusu uwezekano wa kuongezeka mashambulizi yanayowalenga Waislamu nchini humo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jul 03, 2017 08:25 UTC
  • Waislamu Ufaransa watahadharishwa kuhusu ongezeko la mashambulizi ya kigaidi

Viongozi wa makundi na jumuiya mbalimbali za Kiislamu nchini Ufaransa wamewatahadharisha wafuasi wa dini hiyo kuhusu uwezekano wa kuongezeka mashambulizi yanayowalenga Waislamu nchini humo.

Viongozi hao ambao wamelaani shambulizi lililofanyika usiku wa kuamkia leo karibu na Msikiti wa  Arrahma eneo la Avignon kusini mwa Ufaransa, wamewataka Waislamu nchini humo kuwa macho zaidi. 

Viongozi wa jumuiya za Kiislamu Ufaransa pia wamewataka maafisa wa serikali ya Paris kufanya uchunguzi wa kina kuhusu shambulizi hilo na kuzidisha ulinzi kandokando ya vituo vya kidini.

Watu 8 wamejeruhiwa katika shambulizi lililofanywa na watu wawili wasiojulikana dhidi ya watu waliokuwa wamemaliza ibada ya Swala karibu na Msikiti wa  Arrahma eneo  la Avignon.

Wito wa viongozi wa Kiislamu nchini Ufaransa umetolewa baada ya mwendesha mashtaka wa eneo la Avignon kudai kuwa, shambulizi lililolenga Waislamu karibu na msikiti huo halikuwa la kigaidi. 

Msikiti wa Paris, Ufaransa

Shambulizi la kulengwa Waisalmu kwa risasi huko Avignon limeibua wasiwasi miongoni mwa Waislamu Ufaransa ambao hivi karibuni walishuhudia mtu moja akijaribu kuwakanyaga Waislamu kwa gari nje ya msikiti mmoja kusini mashariki mwa Paris.