Feb 17, 2016 15:11 UTC
  • Jela ya wenye misimamo mikali kujengwa Kenya

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema njia pekee ya kupunguza kuenea athari mbaya za ugaidi na madudu yake ni kupitia kuundwa jela ya aina yake itakayotumiwa kuwafungia watu wenye misimamo mikali.

Rais Kenyatta amesema kuchanganyika wafungwa wa kawaida na wale wenye misimamo mikali na magaidi kumechangia tatizo hilo kuenea na watu wengi kujiunga na makundi ya aina hiyo.

"Tutaunda jela maalumu kwa ajili ya watu wenye misimamo mikali. Hatutokubali fikra za ugaidi na misimamo mikali kuenezwa kupitia jela za nchi hii" amesema kiongozi huyo.

Ingawa hakutaja kundi lolote moja kwa moja, wachambuzi wanasema kundi la kigaidi la Boko Haram ndilo lililolengwa kwenye kauli hiyo ya Rais wa Kenya.

Kundi hilo limekuwa likifanya mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya raia na maafisa wa usalama wa Kenya ndani na nje ya nchi hiyo. Shambulizi la hivi karibuni la kundi hilo dhidi ya Kenya ni lile lililotokea katika kambi ya el-Adde ambako wanajeshi zaidi ya 50 kutoka Kenya waliuawa.

Tags