Bunge la Ulaya: Uingereza ianze mchakato wa kuondoka EU
https://parstoday.ir/sw/news/world-i10033-bunge_la_ulaya_uingereza_ianze_mchakato_wa_kuondoka_eu
Spika kwa Bunge la Ulaya ametaka kuanza mchakato wa kuondoka Uingereza katika Umoja wa Ulaya.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jun 26, 2016 23:59 UTC
  • Bunge la Ulaya: Uingereza ianze mchakato wa kuondoka EU

Spika kwa Bunge la Ulaya ametaka kuanza mchakato wa kuondoka Uingereza katika Umoja wa Ulaya.

Martin Schulz Spika wa Bunge la Ulaya amemtaka David Cameron Waziri Mkuu wa Uingereza aanze mchakato wa kuiondoa nchi hiyo katika Umoja wa Ulaya kuanzia Jumanne wiki hii.

Spika wa Bunge la Ulaya ameeleza kuwa kuna wasiwasi kwamba hatua hiyo ya Uingereza itasababisha ukosefu wa utulivu na soko la ajira kuwa hatarini.

Martin Schulz amesema wanataraji kuwa serikali ya Uingereza itatekeleza ahadi zake kuanzia sasa.

Vyama vinne vikuu katika bunge la Ulaya pia vimeandaa rasimu na kumtakak David Cameron aanze mchakato wa kuondoka nchi hiyo katika Umoja wa Ulaya kuanzia Jumanne wiki hii.

Kikao cha Marais na Mawaziri Wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kitakachochunguza kura ya maoni kuhusu kujiondoa Uingereza ndani ya Umoja wa Ulaya kimepangwa kufanyika Jumanne wiki hii huko Brussels mji mkuu wa Ubelgiji.