May 01, 2024 02:23
Sambamba na kuongezeka uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ kutoa hukumu ya kukamatwa maafisa kadhaa wa utawala wa Kizayuni kwa tuhuma za kufanya jinai za kivita huko Gaza, gazeti la Times lilimeandika kuwa, kuna uwezekano pia kwamba Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC inajiandaa kutoa hati ya kukamatwa Netanyahu na maafisa wengine wa ngazi za juu wa Israel akiwemo Waziri wa Vita, Mkuu wa Majeshi na baadhi ya maafisa wa usalama wa utawala huo kwa kuhusika na vita hivyo.